Swali-1. Wakati mwingine najiuliza kama kweli Mungu ananipenda. Kama yeye ni Mungu wa upendo, kwa nini basi kuna mateso na huzuni nyingi duniani?
Jibu: Katika kitabu cha Mungu kiitwacho Biblia Mungu anaeleza bayana kuwa dhambi zetu ndio chanzo cha mateso na huzuni zote. Ni kweli kuwa Mungu anadhihirisha upendo wake katika ulimwengu wote, kama tunavyosoma katika moja ya mistari mingi inayonukuliwa katika Biblia.
Lakini Mungu anayo mengi zaidi ya kusema:
Swali-2. Lakini mimi sio mtu mwovu. Mimi ni mtu mwema na mwadilifu. Wema wangu unazidi ubaya wote niliowahi kufanya. Sasa, hii mistari inanihusu vipi mimi?
Jibu: Kupitia kanuni ya haki ya Mungu hata mtu mwadilifu sana anatazamwa na Mungu kama mtu mwenye dhambi asiye na tumaini katika njia yake kuelekea Jehanum. Biblia hufundisha kwamba hakuna mtu hata mmoja aliye mwema vya kutosha kwa matendo yake mwenyewe anayestahili kwenda mbinguni. Badala yake sisi sote ni watenda dhambi, na wote tuna hatia mbele za Mungu.
Swali-3. Kama mimi ni mtu mwovu kiasi hicho mbele za Mungu, je Mungu atanifanya nini?
Jibu: Biblia hufundisha kwamba mwishoni mwa ulimwengu watu wote waovu watakuja chini ya adhabu ya mwisho ya Mungu katika sehemu inayoitwa Jehanum katika dunia hii na huu muda umekaribia sana. Kuna ushahidi mwingi wa Biblia kwamba kunyakuliwa kwa waamini kutatokea tarehe 21 Mei, 2011, na huu ulimwengu utakoma kuwapo tarehe 21 Oktoba, 2011. Tafadhali wasiliana na Redio ya Familia kwa ajili ya vitabu vya bure, “Wakati Una Mwisho,” na “Tumekaribia Hapo” vitabu vinavyotoa habari nyingi za Biblia kuhusu ratiba na hukumu ya mwisho wa ulimwengu
Swali-4. Ah! Acha mzaha bwana! Kwa hakika hali siyo mbaya kiasi hicho. Kwa hakika Mungu hamaanishi kwamba atamwangamiza mwanadamu na kuichoma dunia, je ndivyo anavyomaanisha?
Jibu: Kwa hakika Mungu anamaanisha kwamba utakuwa wakati unaotisha pindi Anapoifanya dunia hii kuwa Jehanum halisi kwa miezi 5. Kisha Mungu ataangamiza dunia hii na kila kitu kilichomo ndani yake kwa moto.
Swali-5. Hiyo ni hatari! Kwa nini Mungu amwangamize mwanadamu?
Jibu : Kwa sababu Mungu alimwumba mwanadamu ili awajibike kwa Mungu kwa ajili ya matendo yake. Haki kamili ya Mungu inadai malipo kwa ajili ya dhambi.
Swali-6. Jinsi gani inavyotisha! Je Biblia inatoa tumaini lo lote ambapo mtu anaweza kuepuka maangamizo?
Jibu: Kwa hakika inatoa tumaini; kuna mtu ambaye ni mbadala katika kubeba adhabu ya uchungu na angamizo lenye kutisha kwa ajili ya dhambi zetu. Huyo mtu ni Mungu Mwenyewe, ambaye alikuja duniani kama Yesu Kristo ili kubeba ghadhabu ya Mungu kwa ajili ya wale wote aliokuja kuwaokoa.
Swali-7. Je unasema kwamba kama Kristo ni mbadala wangu, Mmoja ambaye aliadhibiwa kwa ajili ya dhambi zangu, hapo nitatakiwa kutokuwa na hofu juu ya kuangamizwa?
JIbu: Ndiyo, hii ni kweli! Kama nimeokolewa, basi Kristo kama mbadala wangu ametoa malipo kwa ajili ya dhambi zangu.
Swali-8. Lakini je inamaanisha nini kumwamini Kristo? Kama ninakubaliana na yote ambayo Biblia inasema juu ya Kristo kama Mwokozi, je hapo nakuwa nimeokolewa kutokana na kuangamizwa milele?
Jibu: Kumwamini Kristo kunamaanisha mambo mengi zaidi ya kukubali kweli za Biblia akilini mwangu. Inamaanisha kwamba nimekuja kuamini Biblia nzima kama kitabu cha Sheria ya Mungu kwangu. Pia inamaanisha kwamba nina nia kubwa inayoendelea katika kutii maagizo yote ya Biblia. Hivyo nakuwa na furaha kabisa wakati ninapoishi kwa jinsi Mungu anavyonielekeza ndani ya Biblia.
Swali-9. Unasema kwamba hakuna njia ninayoweza kuepuka hayo maangamizi isipokuwa kupitia kwa Yesu? Vipi kuhusu dini nyingine? Je wafuasi wao pia wataangamizwa?
JIbu: Naam! Hawawezi kuepuka ukweli kwamba Mungu anatuwajibisha kwa ajili ya dhambi zetu. Mungu anadai kwamba tutoe malipo kwa ajili ya dhambi zetu. Dini nyingine, pamoja na watu wengi wanaotumia jina la Yesu Kristo, hawawezi kutoa mbadala au mtu wa kuchukua nafasi ya kubeba dhambi za wafuasi wao. Kristo ndiye pekee anayeweza kubeba hatia na aibu yetu na kutuokoa. Kwa hiyo imempasa kila mtu kuiacha dini yake na kuja kuiamini Biblia peke yake.
Swali-10. Sasa nimekata tamaa. Sitaki kwenda kuangamizwa. Je nifanye nini ili nipate kuokoka?
Jibu: Hakuna lo lote unaloweza kufanya ili kujiokoa mwenyewe. Biblia inatwambia kwamba Mungu peke yake ndiye anayeweza kutuokoa. Mungu hufanya muujiza mkubwa wa wokovu kwa kutumia Neno la Mungu (Biblia) katika mioyo na maisha ya wale anaopanga kuwaokoa. Matokeo ya huu muujiza wa wokovu katika maisha ya mtu aliyeokolewa ni kwamba sasa hivi huyo mtu ana upendo kwa Mungu na Biblia. Sasa hivi anafurahi wakati anapotii kitabu cha Sheria ya Mungu, Biblia. Hivyo, kama kweli mtu anatamani kuokolewa lazima atumie muda mwingi kwa makini akisoma au kusikiliza Biblia.
Swali-11. Unaendelea tu kuinukuu Biblia. Biblia ni muhimu kiasi gani?
Jibu. Biblia ni kitabu muhimu sana ulimwenguni kwa sababu ni kitabu cha Sheria ya Mungu kwa wanadamu wote. Kwa kusoma au kusikiliza Biblia mtu anakuwa katika sehemu ambapo Mungu anaweza kumwokoa kama hayo ni mapenzi ya Mungu kwa mtu huyo. Kadhalika atajifunza kweli nyingi nzuri na za ajabu kuhusu Mungu, ghadhabu ya Mungu na mpango wa wokovu wa Mungu. Kwa hakika anasikiliza sauti ya Mungu kwa sababu Mungu ndiye mwandishi wa Biblia na kwa hiyo anaongea naye kupitia Maneno yake (Biblia)
Swali-12. Je, ninaweza kumwomba Mungu anirehemu na kuniokoa?
Jibu: Kwa hakika NDIYO! Mungu ni mwenye rehema sana. Kwa hiyo, Biblia inatwambia kwamba tunaweza na inatupasa kumwomba, kumlilia ili aturehemu na kutuokoa, huku tukitambua ya kuwa sisi ni watenda dhambi tunaostahili ghadhabu ya Mungu. Hii haitatuokoa, ila tutakuwa na uhakika kwamba Mungu anafahamu nia yetu kubwa ya kutaka kuokolewa.
Swali-13. Je, inanipasa kuhudhuria kanisani?
Jibu: Kwa hakika HAPANA! Biblia inatuambia kwamba kwa karibu miaka 2000 baada ya Yesu kufa msalabani, wale waliomwamini Yesu, kama ingewezekana, iliwapasa kuwa wanachama wa kanisa. Lakini leo tunajifunza kutoka kwenye Biblia ya kuwa Mungu haokoi tena watu kupitia huduma ya makanisa. Kipindi cha kanisa kimefika mwisho. Ukweli ni kwamba Mungu anaamuru katika kitabu Chake cha Sheria, Biblia, ya kwamba waamini wa kweli wanatakiwa kuliacha kanisa lao. Hii ni kwa sababu Hukumu ya Mungu yenye haki ipo juu ya mikusanyiko yote ya waumini wakati Mungu anapouandaa ulimwengu kwa ajili ya Siku ya Hukumu.
Ni lazima tukumbuke kuwa hatuwezi kuokolewa na kanisa au mchungaji, au padre, au kwa ubatizo wa maji, au meza ya Bwana. Yesu Kristo peke yake ambaye ni Mungu Mwenyewe, ndiye anayeweza kutuokoa. Biblia inafundisha kwamba kwa wakati huu, ambapo tumekaribia sana na mwisho wa wakati, hapo ni nje ya makanisa ambapo Mungu anaokoa mkutano wa watu wengi sana.
Unaweza kupokea vitabu vya bure kutoka Redio ya Familia bila gharama au masharti yo yote “Mwisho wa Nyakati za Kanisa na Baada” na “Ngano na Magugu” Vinatoa ujumbe mwingi wa Kibiblia ambao unaonyesha kwamba tumefika mwisho wa nyakati za kanisa.
Swali-14. Tafadhali nieleze zaidi jinsi Mungu anavyookoa watu.
Jibu. Biblia katika Yohana 11 inatupa mfano mzuri sana unaoonyesha kwamba Mungu peke yake anafanya kazi yote ya kutuokoa. Kristo alimfufua mwanaume aliyeitwa Lazaro ambaye alikuwa amekufa kwa siku nne. Yesu alisimama nje ya kaburi la Lazaro na kuamuru “Lazaro, njoo huku nje.” Ni wazi kuwa maiti iliyokuwa imeoza ndani ya kaburi isingeweza kumsikia Yesu au kumtii.
Lakini Lazaro alisikia agizo la Yesu na alitoka nje ya kaburi, akiwa mtu hai. Hiyo ilitokeaje? Ilimaanisha kwamba wakati Yesu alipomwamuru Lazaro aliyekuwa amekufa kutoka nje, Yesu katika Roho Yake alitakiwa kuingia ndani ya lile kaburi na kuipa uhai wa mwili ile maiti iliyokuwa inanuka, kuipa masikio iweze kusikia, na utashi pamoja na nguvu ili kutii agizo la Kristo.
Biblia inatwambia kwamba kabla hatujaokolewa tunakuwa tumekufa kiroho. Bado Mungu anatuamuru kumtafuta Mungu, kuamini na kutubu. Walakini, kama ambavyo haikuwa rahisi kwa Lazaro aliyekuwa amekufa kutii agizo la Yesu kutoka nje ya kaburi, siyo rahisi kwa mtu aliyekufa kiroho kutii agizo la Mungu kumwamini Yesu kwa ajili ya wokovu.
Kadhalika kwa wale ambao Mungu amepanga kuwaokoa, wakati Anapotuamuru kuamini, kutubu na kupata kuokolewa, Anaongea na wafu wa kiroho ambao kwao wenyewe kamwe wasingeweza kujiokoa. Lakini kuna wale ambao wanaanza kumwamini Kristo kama Mwokozi, wanaotambua kuwa na furaha kuu wakati wanapofanya mapenzi ya Mungu. Ushahidi upo katika maisha yao kwamba kwa njia moja au nyingine walipata kuokolewa. Hii inaweza tu kutokea kwa sababu wakati Mungu anapowaamuru kuamini, pia Mungu anaingia ndani ya maisha yao na kuwaokoa. Kwa sababu Mungu aliwaokoa, walitambua kuwa walipata kumwamini Yesu. Walitambua kwamba dhambi ilikuwa mbaya sana kwao. Ilikuwa ushahidi kwamba Mungu aliwachagua wapate kuokolewa. Wakati aliposikia Injili, Mungu alitumia Neno la Mungu katika maisha yao na wakapata kuokolewa. Kama haujaokolewa sikiliza Biblia kwa bidii. Kwa makini na kwa kuomba soma na isome Biblia. Inawezekana na wewe pia ukapokea wokovu wakati Mungu anapokuita kupitia kitabu chake cha Sheria, Biblia.
HAIDHURU UMEISHI MAISHA MABAYA SANA KIASI GANI AU JINSI ULIVYOTENDA DHAMBI SANA, INAWEZEKANA KABISA KWAMBA KWA REHEMA ZA MUNGU WEWE PIA UMECHAGULIWA NA MUNGU KUOKOLEWA.
Lakini kumbuka ya kuwa Mungu hufanya kila kitu kwa wakati wake. Kwa hiyo umsubiri Mungu kwa unyeyekevu wakati unaendelea kujifunza kutoka kwenye Biblia.
Kwa kupata bure mwongozo wa vipindi vyetu vya matangazo ya Injili, habari kuhusu kupata bure mafundisho yetu ya Biblia kwa njia ya posta (Kiingereza), au vitabu vya bure, na vifaa tuma barua kwa:
Barua pepe: International@familyradio.com
Katika Mtandao: http://www.familyradio.com
Redio ya Familia ni huduma ya matangazo ya Kikristo yenye misingi ya Biblia pasipo kushirikisha kanisa.